Saturday, June 3, 2023

NJIA ZA KUPATA MTAJI WA BIASHARA

 PART 1

NJIA ZA KUPATA MTAJI WA BIASHARA

Baada ya kuamua kuingia kwenye biashara/ ujasiriamali, sasa unahitaji mtaji wakufanyia na kukuzia biashara yako.

Mambo muhimu kuyajua:Sio kila biashara inahitaji mtaji au mtaji mkubwa! Kuna biashara zingine unahitaji tu kufahamiana na watoa bidhaa au huduma basi. Mfano biashara ya bodaboda, unahitaji tu kufahamiana na mwenye boda boda wewe unafanya kazi kwanza halafu unapeleka sehemu ya makubaliano yako na tajiri baadaye

Hata kama biashara yako itahitaji mtaji mkubwa unaweza siku zote funja funja hayo malengo ya biashara katika ngazi ambayo unaweza anza na mtaji unaoweza kumudu kuupata.Mfano unaweza kuwa unataka kuwa na hoteli kubwa ya biashara. Hapa unaweza anza na mgahawa na baadaye ikakua Mfano wa pili Labda unataka kuwa na supermarket, unaweza anza na mtaji wa 10,000 kuunza vitunguu, chumvi kwa nyumba za jirani mpaka ufukishe mwaka utakuwa na mtaji mkubwa ajabu.


Kama biashara yako itahitaji mtaji kwanza fikiria mambo manne (4) yafuatayo

1. Aina ya biashara (Kuzalisha, kuchuuza, huduma)

2. Aina ya soko (kipato kidogo, wanawake tu, wanaume tu, watoto tu, vijana tu, kijiji au mtaa tu nk)

3. Ukubwa wa mtaji (Mdogo, wa kati au mkubwa?)

4. Ufahamu wako kwenye biashara yako – Elimu/Ujuzi nk

Majibu ya maswali hapo juu ndio itakayoamua wewe upate mtaji wapi


Sasa swali, wapi utapata huo mtaji

1. Mali Binafsi

Kama una shamba, fedha, nyumba, gari, mifugo, mazao nk unaweza kutumia mali hizi kama mtaji wa biashara

Kumb. Ukishakubali kuwa mfanyabiashara wewe utakuwa daima ni mtu wa kununua na kuuza. Kwa hiyo hata kitanda chako unachokipenda sana kwa wakati fulani unaweza lazimika ukiuze ili upate mtaji wa biashara. Muhimu usiingie kichwa kichwa kwenye biashara na kujiletea hasara.


Faida ya aina hii ya mtaji#Haina riba, hata ikitokea bahati biashara ikafilisika haiwezi filisi na mali zingine kwani hakuna dhamana ya mali yako.


Hasara:# Hakuna msukumo wa biashara kwani mhusika hajali hata akipata hasara, Hivyo ni vigumu kupata faida na biashara kukua.


2. Wabia wa Biashara

Saa nyingine unatakiwa kuwatumia watu wengine ili kupata yafuatayo

1. Mtaji wa mali

2. Mtaji wa mawazo na fikra tofauti

Wabia wa baishara yako inaweza ongeza kasi ya kukua kwa biashara kwani fikra tofauti inaweza kuwa chachu ya maendeleo ya biashara husika ukiachilia mbali mtaji ambao wabia wako watakuja nao.

Inabidi lakini uwachague kwa uangalifu mkubwa wabia wako kwani wengine wanaweza kuwa ni wavurugaji na sio wa kuaminiwa.


Faida: Kuongezeka kwa kasi ya kukua kwa biashara kwa sababu ya fikra tofauti


Hasara: Mifarakano yenye kuweza kuua biashara ni dhahiri


3. Wawekezaji wa Biashara

Wawekezaji ni watu ambao wanaweza toa mali na pesa zao kukuwezesha wewe kufanya biashara yako lakini wao watahitaji baada ya muda wa uwekezaji warudishiwe pesa au mali zao na riba mliokubaliana kwenye mktaba wa uwekezaji.


Faida: Uhakika wa mtaji na hivyo uhakika wa kufanya biashara


Hasara: Biashara isipotengeneza faida kwa muda mliokubaliana inaweza sababisha kushitakiana na hatimaye biashara na mali zako kufilisiwa


4. Mkopo Kutoka kwa Watu wa Karibu

Ndugu/jamaa/marafiki na majirani wanaweza kuwa ni chanzo kizuri ya mtaji usio nariba.

Wanaweza kukupa fedha taslimu, wanyama, vitu kama mashine, mitambo, nyumba, ardhi, gari, kompyuta, na vifaa mbalimbali


Faida: Ni rahisi kupata mkopo bila mlolongo wa masharti, uwezekano wa kufilisiwa ni mdogo au hakuna kabisa


Hasara: Kwa vile ni mkopo wa ndugu/jamaa, jirani na marafiki, hakuna msukumo wa kufanya biashara kwa sababu hakuna kufilisiwa hivyo ni ngumu kupata faida na pia kukua kwa biashara yako


#SOMOLITAENDELEA

#SHARENAMWENZAKOAJIFUNZEPIA

NJIA ZA KUPATA MTAJI WA BIASHARA

 PART 2

somo lililopita tulijifunza njia nne za kupata mtaji wa biashara pamoja na faida na hasara za kila njia. Sasa tunaendelea na njia zingine za kupata mtaji wa biashara


5. Mkopo Kutoka Kwenye Vyama, Vikundi nk

Vyama vya kijamii, kitaaluma, vikundi vya kuweka na kukopa, Vikoba vinaweza kuwa chanzo cha karibu kupata mkopo wa biashara wenye riba na masharti nafuu. Unachotakiwa tu ni kuwa mwanachama wa chama chenye kukopesha na kufuata masharti ya chama husika.


Faida: Uhakika wa mtaji japo unaaza na mdogo, uanweza kuepuka kufilisiwa mali zako. Kunakuweo na msukumo kwa kiwango fulani ya kufanya biashara na hivyo uwezekano wa kupata faida na biashara yako kukua


Hasara: Mtaji ni mdogo pale unapooanza


6. Mkopo Kutoka Kwenye Mashirika ya fedha (Micro-Credit Enterprises)

Mashirika kama Pride Tanzania, Vision Tanzania (zamani ikiitwa SEDA), Finca, Faida nk ni hatua nzuri kwa biashara ndogo kwani nao kama ilivyo vikoba wanatoa mikopo midogo kwa masharti nafuu.


Faida: Mlolongo mdogo, dhamana ni rahisi, wanaelimisha


Hasara: Riba ni kubwa, biashara ikifeli utafilisiwa mali ulizoweka dhamana


7. Mkopo kutoka Benki na Tasisi kubwa za Fedha

Mkopo unaohusisha benki ni sharti iwe ni biashara kubwa na mhusika awe na uhakika na soko pamoja na mtaji kurudi.

Mabenki mengine wanatoa mikopo mikubwa na midogo kwa pamoja.


Faida: Uhakika wa kupata mkopo mkubwa, pia msukumo wa kufanya biashara ni mkubwa na hivyo uwezekano mkiubwa wa kutengeneza faida


Hasara: Mlolongo wa kuupata ni mrefu, Kwa bahati mbaya biashara ikifeli, unafilisiwa haraka mali uliyoweka dhamana


Masharti ya mkopo

Unapokwenda benki  au taasisi nyingine za kifedha kuomba mkopo lazima utakutana na masharti yafuatayo ili uweze kupata mkopo huo. 

– Dhamana kama vile nyumba, arthi, mazao, kikundi n.k.

– Mchanganuo wa biashara

– Biashara inayo endelea(<miaka 3)

– Kuwepo kwa ofisi kama ni mkopo mkubwa zaidi ya milioni 3

– Biashara iliyosajiliwa kam ni biashara kubwa

– Riba ya mkopo

– Kiasi cha mkopo na uwezo wa mkopo

– Muda wa kurudisha mkopo na riba

#MWISHOWASOMO #SHARENAMWENZAKOAJIFUNZEPIA

NJIA MUHIMU ZA KUWAVUTIA WATEJA

 PART I



Tuangalie baadhi ya njia ambazo zinaweza kutumika ili kuwavuta wateja katika shughuli mbalimbali zinazofanywa na wajasiriamali. Ikumbukwe njia hizi ni baadhi kati ya nyingi ambazo zinaweza kujenga ufanisi na kuwezesha biashara kusonga mbele.


1. Fanya utafiti wa mahali pazuri pa kufanyia biashara.Eneo ambalo biashara ipo ni jambo la msingi sana katika kuwavutia wateja na kujenga ufanisi katika biashara. Ni vyema pia kutambua si kila biashara inafaa kwa kila eneo na vilevile si kila eneo linafaa kwa kila biashara!

Unaweza kulalamika kwamba biashara sio nzuri na mambo hayaendi lakini kumbe mwanzo wa yote ni biashara yenyewe kutokuwa kwenye eneo sahihi, haya ni makosa yanayofanywa na wajasiriamali wengi hivyo chagua eneo sahihi kwaajili biashara yako. Inawezekana upatikanaji wa maeneo ya biashara hasa maeneo mazuri yanahusisha gharama kubwa katika upatikanaji wake, ni muhimu ufanye tathmini ya uhusiano wa eneo na aina ya biashara unayotegemea kufanya.


2. Tambua wateja halisi wa biashara yako.

Je ni wapita njia? Unapoamua kufanya biashara fikiria pia juu ya walengwa halisi wa biashara husika, ingawa wanaweza kutokea wateja mbalimbali lakini lazima walengwa wawepo.

Elewa wateja ni msingi wa mafanikio katika biashara yako, jiulize wateja wako ni akina nani, nini kitawasukuma kuja kununua kwako, je ni watu wenye uwezo wa kifedha kwa kiasi gani na wanatoka wapi? Ukijiuliza maswali haya utaweza kufahamu namna ya kubuni biashara nzuri kwaajili ya wateja wako.Kwa mfano ukienda benki kuna akaunti za aina mbalimbali kutokana na madaraja ya wateja, kuna akaunti za makampuni, akaunti za watoto n.k. Hivi ndivyo na wewe kama mjasiriamali unatakiwa kufikiria kuhusu aina ya wateja wako.

Ni muhimu kuwa na mchanganuo wa aina mbalimbali za wateja unaowalenga katika bishara yako. Haiwezekani ‘’nguo’’ moja ikamtosha kila mtu! Kwa mfano kama umeamua kufungua duka la nguo jiulize walengwa ni kina nani na utawapataje?Kumbuka soko ni kubwa sana na wateja ni wengi, hivyo wewe kama mjasiriamali unatakiwa kuwaainisha wateja wako katika matabaka kutokana na aidha mila, desturi, uwezo wa kiuchumi, jinsia, elimu, au maeneo wanayotoka.


3. Ainisha bei stahiki ya bidhaa zako.

Ni muhimu kwa mjasiriamali kupanga bei za bidhaa zake kwa namna ambayo itawaridhisha wateja. Pamoja na kuwa na soko la bidhaa zako, yakupasa kuwa na bei zenye kukubalika miongoni mwa wateja wako.Vilevile angalia uwezo wa kiuchumi wa eneo husika, zipo baadhi ya bidhaa ambazo bei zake zinaeleweka na zipo bidhaa ambazo bei zake hutofautiana kutokana na mahali. Hii yote inatokana na uwiano wa kiuchumi, mila, desturi na tamaduni za jamii husika.Kuna changamoto kubwa katika upangaji wa bei za bidhaa, hii ni kwasababu mara nyingi bei huwakilisha aidha gharama za uzalishaji wa bidhaa au thamani ya bidhaa husika. Inashauriwa kuwa ni vyema mjasiriamali asijifunge katika upangaji wa bei za bidhaa zake na badala yake acheze na soko.


SOMOLITAENDELEA

SHARENAMWENZAKOAJIFUNZEPIA

Thursday, June 1, 2023

UWE NA MOYO WA UJASIRI

 UWE NA MOYO WA UJASIRI


Moyo wa ujasiri ni moyo uliojaa imani thabiti, ni moyo usiokata tamaa,  naam ni moyo usiyoyumbishwa na changamoto zinazotokea katika maisha, moyo huo ndiyo yatupasa tuwe nao ili tuweze kushinda katika safari yetu hapa duniani.


kila wakati jifunze kuwa na moyo wa ujasiri kwenye kila kitu unachofanya au unachotaka kufanya ili kuzifikia ndoto zako, usihofu kuhusu changamoto zinazojitokeza au zitakazojitokeza katika eneo ulilopo kwa sasa.


Elewa kwamba kila changamoto na ugumu ambao unakutana nao leo unasababu kubwa sana kama utatuliza akili yako na kutafakari juu ya ugumu huo. Haupaswi kukataa tamaa kwa sababu ya changamoto zinazojitokeza. 


Mara nyingi ugumu wa jambo fulani huwa una fumbo, ni vyema ukaelewa kwamba changamoto hazipo kukuangamiza bali zipo kukuimarisha kiimani na kisha uende viwango vingine.


 Kila hali ngumu unayokutana nayo leo ili hali hiyo uweze kuishinda yakupasa ujivika imani ya ujasiri kwa kumtegemea Mungu, wenda ni katika kazi, biashara, mahusiano n.k.


Epuka hali ya kukataa tamaa kwa sababu kila jambo lina ugumu wake hakuna jambo ambalo linapatiakana kiurahisi kama uzaniavyo, maana nyuma ya changamoto unazozipitia kuna mafanikio makubwa sana.


Nakusihi sana Rafiki yangu uwe JASIRI pale ukutanapo na hali ya ugumu katika kila jambo ufanyalo kwa kumshirikisha Mungu kila hatua upigayo, katu usirudi nyuma bali songa mbele.


Tambua wewe ni shujaa hivyo usikatishwe tamaa na changamoto mbalimbali unazokumbana nazo huwapo katika harakati za kuyafanikisha maono yako.


Neno la Mungu linatuhasa tuwe majasiri na hodari katika maisha, linasema:-


"...Uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa BWANA, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako." (Yoshua 1:9)


Moyo wa ujasiri unapatikana kwa kutambua ya kuwa Mungu yu pamoja nawe katika kila ufanyalo na katika kila mahali uendako, hivyo usiogope chochote kile mpendwa, wewe chapa kazi kwa bidii huku ukimtegemea Mungu na kila kitu kitakuwa sawa tu.


MUHIMU: "Usiombe maombi ya kuyafanya maisha yawe rahisi kwako, bali omba maombi ya kupata ujasiri na uhodari (uimara), maana uimara utakupa nguvu za kushinda kwenye huohuo ugumu uliopo kwenye maisha."


Kwa Mafundisho zaidi tembelea ukurasa huu ๐Ÿ‘‡๐Ÿฟ

https://biashara-news.blogspot.com?m=1

Pia nakuomba SHARE ujumbe huu kwa wengine nao wajifunze pia.


Nakutakia siku njema.

List of Documents required for Exports Customs Clearance

 Importation means goods and services brought to Tanzania from a foreign country.

 Import as been followed under the good and services from custom control as per East Africa comunity customs management act.(EACCMA 2004). 

Tanzania import are subjected to different stages where by importers is advised to make declaration through of appointing clearing and forwarding agent lodging documents at least seven (7) days before the arrival of the prior vessel.

The following are the documents used in importation.

1. Agent's authorization letter from the importer; this is one of the document used in importation of goods and services there should be agent authorization letter by importer.

2. Bills of entry; This is legal documents to be filled and signed by an importer. It is filled and signed then other necessary documents, assessment and examination of goods are carried out by authority. And offer completing the process an importer can avail for ITC claim on goods.

3. Import license; this is a permission granted by the government to undertake import activities for restricted goods. So, one must file an application to the license authority in order to avail the benefits.

4. Insurance certificate. This is documents required for import customs clearance. This helps authorities to verify the shipment in terms of whether the selling price contains the insurance or not. Also it helps to determine the precise value which eventually decides the import duty aggregate.

5. Technical write up, literature. This is documents which is only required for some specific goods. It describe the features and usage of the products, mostly done for better handling of goods. This documents helps the authority to better define the product and understand the value-added cost under it.

6. Industrial license. This documents also is required for importation of specific commodities. An industrial license can be used as proof to avail the benefit, if an importer wants to avail any import duty benefit.

7. Packing list. This is also the documents used in importation of goods and services, is the one to select the type of document and a means of transportation either the goods to be transported through airways or land through vehicles.

8. Importation permits from TFDA and TBS; when importing goods in Tanzania there are some of the authorities which are dealing with importation we can take a look in Tanzania we have TBS which looks the standards of goods to be imported and exported.

Generally, After obtaining the importation document the importer through different authorities like TANCIS and TBS will give them an access of importing goods and services and importation has got a great advantages to individual and the Nation at all in individual level gives people source of income and improves the living standards of an individual, while in national level it gives availability of goods and services, also build relationship between Nations.

Ad