Saturday, June 3, 2023

NJIA MUHIMU ZA KUWAVUTIA WATEJA

 PART I



Tuangalie baadhi ya njia ambazo zinaweza kutumika ili kuwavuta wateja katika shughuli mbalimbali zinazofanywa na wajasiriamali. Ikumbukwe njia hizi ni baadhi kati ya nyingi ambazo zinaweza kujenga ufanisi na kuwezesha biashara kusonga mbele.


1. Fanya utafiti wa mahali pazuri pa kufanyia biashara.Eneo ambalo biashara ipo ni jambo la msingi sana katika kuwavutia wateja na kujenga ufanisi katika biashara. Ni vyema pia kutambua si kila biashara inafaa kwa kila eneo na vilevile si kila eneo linafaa kwa kila biashara!

Unaweza kulalamika kwamba biashara sio nzuri na mambo hayaendi lakini kumbe mwanzo wa yote ni biashara yenyewe kutokuwa kwenye eneo sahihi, haya ni makosa yanayofanywa na wajasiriamali wengi hivyo chagua eneo sahihi kwaajili biashara yako. Inawezekana upatikanaji wa maeneo ya biashara hasa maeneo mazuri yanahusisha gharama kubwa katika upatikanaji wake, ni muhimu ufanye tathmini ya uhusiano wa eneo na aina ya biashara unayotegemea kufanya.


2. Tambua wateja halisi wa biashara yako.

Je ni wapita njia? Unapoamua kufanya biashara fikiria pia juu ya walengwa halisi wa biashara husika, ingawa wanaweza kutokea wateja mbalimbali lakini lazima walengwa wawepo.

Elewa wateja ni msingi wa mafanikio katika biashara yako, jiulize wateja wako ni akina nani, nini kitawasukuma kuja kununua kwako, je ni watu wenye uwezo wa kifedha kwa kiasi gani na wanatoka wapi? Ukijiuliza maswali haya utaweza kufahamu namna ya kubuni biashara nzuri kwaajili ya wateja wako.Kwa mfano ukienda benki kuna akaunti za aina mbalimbali kutokana na madaraja ya wateja, kuna akaunti za makampuni, akaunti za watoto n.k. Hivi ndivyo na wewe kama mjasiriamali unatakiwa kufikiria kuhusu aina ya wateja wako.

Ni muhimu kuwa na mchanganuo wa aina mbalimbali za wateja unaowalenga katika bishara yako. Haiwezekani ‘’nguo’’ moja ikamtosha kila mtu! Kwa mfano kama umeamua kufungua duka la nguo jiulize walengwa ni kina nani na utawapataje?Kumbuka soko ni kubwa sana na wateja ni wengi, hivyo wewe kama mjasiriamali unatakiwa kuwaainisha wateja wako katika matabaka kutokana na aidha mila, desturi, uwezo wa kiuchumi, jinsia, elimu, au maeneo wanayotoka.


3. Ainisha bei stahiki ya bidhaa zako.

Ni muhimu kwa mjasiriamali kupanga bei za bidhaa zake kwa namna ambayo itawaridhisha wateja. Pamoja na kuwa na soko la bidhaa zako, yakupasa kuwa na bei zenye kukubalika miongoni mwa wateja wako.Vilevile angalia uwezo wa kiuchumi wa eneo husika, zipo baadhi ya bidhaa ambazo bei zake zinaeleweka na zipo bidhaa ambazo bei zake hutofautiana kutokana na mahali. Hii yote inatokana na uwiano wa kiuchumi, mila, desturi na tamaduni za jamii husika.Kuna changamoto kubwa katika upangaji wa bei za bidhaa, hii ni kwasababu mara nyingi bei huwakilisha aidha gharama za uzalishaji wa bidhaa au thamani ya bidhaa husika. Inashauriwa kuwa ni vyema mjasiriamali asijifunge katika upangaji wa bei za bidhaa zake na badala yake acheze na soko.


SOMOLITAENDELEA

SHARENAMWENZAKOAJIFUNZEPIA

Thursday, June 1, 2023

UWE NA MOYO WA UJASIRI

 UWE NA MOYO WA UJASIRI


Moyo wa ujasiri ni moyo uliojaa imani thabiti, ni moyo usiokata tamaa,  naam ni moyo usiyoyumbishwa na changamoto zinazotokea katika maisha, moyo huo ndiyo yatupasa tuwe nao ili tuweze kushinda katika safari yetu hapa duniani.


kila wakati jifunze kuwa na moyo wa ujasiri kwenye kila kitu unachofanya au unachotaka kufanya ili kuzifikia ndoto zako, usihofu kuhusu changamoto zinazojitokeza au zitakazojitokeza katika eneo ulilopo kwa sasa.


Elewa kwamba kila changamoto na ugumu ambao unakutana nao leo unasababu kubwa sana kama utatuliza akili yako na kutafakari juu ya ugumu huo. Haupaswi kukataa tamaa kwa sababu ya changamoto zinazojitokeza. 


Mara nyingi ugumu wa jambo fulani huwa una fumbo, ni vyema ukaelewa kwamba changamoto hazipo kukuangamiza bali zipo kukuimarisha kiimani na kisha uende viwango vingine.


 Kila hali ngumu unayokutana nayo leo ili hali hiyo uweze kuishinda yakupasa ujivika imani ya ujasiri kwa kumtegemea Mungu, wenda ni katika kazi, biashara, mahusiano n.k.


Epuka hali ya kukataa tamaa kwa sababu kila jambo lina ugumu wake hakuna jambo ambalo linapatiakana kiurahisi kama uzaniavyo, maana nyuma ya changamoto unazozipitia kuna mafanikio makubwa sana.


Nakusihi sana Rafiki yangu uwe JASIRI pale ukutanapo na hali ya ugumu katika kila jambo ufanyalo kwa kumshirikisha Mungu kila hatua upigayo, katu usirudi nyuma bali songa mbele.


Tambua wewe ni shujaa hivyo usikatishwe tamaa na changamoto mbalimbali unazokumbana nazo huwapo katika harakati za kuyafanikisha maono yako.


Neno la Mungu linatuhasa tuwe majasiri na hodari katika maisha, linasema:-


"...Uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa BWANA, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako." (Yoshua 1:9)


Moyo wa ujasiri unapatikana kwa kutambua ya kuwa Mungu yu pamoja nawe katika kila ufanyalo na katika kila mahali uendako, hivyo usiogope chochote kile mpendwa, wewe chapa kazi kwa bidii huku ukimtegemea Mungu na kila kitu kitakuwa sawa tu.


MUHIMU: "Usiombe maombi ya kuyafanya maisha yawe rahisi kwako, bali omba maombi ya kupata ujasiri na uhodari (uimara), maana uimara utakupa nguvu za kushinda kwenye huohuo ugumu uliopo kwenye maisha."


Kwa Mafundisho zaidi tembelea ukurasa huu 👇🏿

https://biashara-news.blogspot.com?m=1

Pia nakuomba SHARE ujumbe huu kwa wengine nao wajifunze pia.


Nakutakia siku njema.

List of Documents required for Exports Customs Clearance

 Importation means goods and services brought to Tanzania from a foreign country.

 Import as been followed under the good and services from custom control as per East Africa comunity customs management act.(EACCMA 2004). 

Tanzania import are subjected to different stages where by importers is advised to make declaration through of appointing clearing and forwarding agent lodging documents at least seven (7) days before the arrival of the prior vessel.

The following are the documents used in importation.

1. Agent's authorization letter from the importer; this is one of the document used in importation of goods and services there should be agent authorization letter by importer.

2. Bills of entry; This is legal documents to be filled and signed by an importer. It is filled and signed then other necessary documents, assessment and examination of goods are carried out by authority. And offer completing the process an importer can avail for ITC claim on goods.

3. Import license; this is a permission granted by the government to undertake import activities for restricted goods. So, one must file an application to the license authority in order to avail the benefits.

4. Insurance certificate. This is documents required for import customs clearance. This helps authorities to verify the shipment in terms of whether the selling price contains the insurance or not. Also it helps to determine the precise value which eventually decides the import duty aggregate.

5. Technical write up, literature. This is documents which is only required for some specific goods. It describe the features and usage of the products, mostly done for better handling of goods. This documents helps the authority to better define the product and understand the value-added cost under it.

6. Industrial license. This documents also is required for importation of specific commodities. An industrial license can be used as proof to avail the benefit, if an importer wants to avail any import duty benefit.

7. Packing list. This is also the documents used in importation of goods and services, is the one to select the type of document and a means of transportation either the goods to be transported through airways or land through vehicles.

8. Importation permits from TFDA and TBS; when importing goods in Tanzania there are some of the authorities which are dealing with importation we can take a look in Tanzania we have TBS which looks the standards of goods to be imported and exported.

Generally, After obtaining the importation document the importer through different authorities like TANCIS and TBS will give them an access of importing goods and services and importation has got a great advantages to individual and the Nation at all in individual level gives people source of income and improves the living standards of an individual, while in national level it gives availability of goods and services, also build relationship between Nations.

Monday, May 29, 2023

Andika hivi matangazo yako ya mtandaoni

 


 


Kuandika matangazo yanayouza bidhaa au huduma yako ni hitaji la kila mfanyabiashara anayefanya matangazo ya kulipia mtandaoni.

 

 

Lakini usichokijua ni kwamba tangazo haliwezi likauza bidhaa au huduma yako.

 

 

Kwasababu kazi ya tangazo sio kuuza bidhaa au huduma yako.

 

 

Kazi ya tangazo ni kukuletea wewe mtu mwenye sifa za kuwa mteja wako ili wewe sasa ndio umgeuze mtu huyo kuwa mteja wako.

 

 

Tangazo lako halina utofauti na chambo kwa mvuvi.

 

 

Kazi ya chambo ni kuvuta na kushawishi samaki ang’ate ndoano.

 

 

Baada ya hapo kazi ni kwako mvuvi umchukue samaki ukamkaange, umchome, umuuze au umfanye vyovyote vile utakavyo.

 

 

Kwahiyo hata tangazo linafanya kazi sawa na chambo.

 

 

Tangazo litamshawishi msomaji akutafute kwa ajili ya kupata bidhaa au huduma yako.

 

 

Mtu akishakutafuta tangazo linakuwa limemaliza kazi yake.

 

 

Kazi yako ni kufanya juu chini mtu huyu aliye kutafuta ananunua bidhaa yako.

 

 

Asiponunua kuna uwezekano wa mambo 2 kutokuwa sawa.

 

 

  1. Hujui mbinu za kumclose mtu kuwa mteja wako

 

  2. Umelenga watu ambao hawana sifa za kuwa wateja wako hivyo tangazo linakuletea watu ambao sio sahihi kwa bidhaa au huduma yako.

 

 

Tuseme unajua kuclose vizuri ila unafeli kwenye uandishi wa tangazo lenye ushawishi kwa msomaji na unashindwa kulenga watu sahihi ili tangazo lako lionekane na lisomwe na watu wenye uhitaji wa bidhaa yako.

 

 

Kama tatizo lako ni hilo nina mashaka na uelewa wako juu ya mteja wako.

 

 

Nina uhakika 75% utakakuwa hujui sifa za mteja wako.

 

 

Fikiria unaongea kiswahili mbele ya mzungu asiyejua hata neno moja la kiswahili.

 

 

Ataishia kukushangaa tu maana atakuwa haelewi unachozungumza ni nini.

 

 

Kwahiyo hatua ya kwanza ya uandishi wa tangazo lenye kumshawishi msomaji kukutafuta ni kumuelewa mteja wako nje ndani.

 

 

Ukimuelewa mteja wako nje ndani ni rahisi kuandika tangazo ambalo linazungumza kwa mlengwa moja kwa moja.

 

 

Na utakachokiandika kwenye tangazo lako sio kuhusu bidhaa yako kwasababu mteja hajali hata robo kuhusu bidhaa au huduma yako.

 

 

Anachojali ni kuhusu yeye na yeye peke yake.

 

 

Kwahiyo utakachokiandika kwenye tangazo lako ni mambo 3.

 

 

Jambo #1: Anachokihitaji mteja.

 

 

Kila mtu anahitaji lake. Hitaji lako sio lake. 

 

 

Nitakuwa na uhitaji wa bidhaa yako endapo utanionesha kwamba kupitia bidhaa au huduma yako nitapata ninachokihitaji.

 

 

Kwahiyo bidhaa au huduma yako ni daraja tu, sio kitu ninachokihitaji.

 

 

Ninachokihitaji ni kile ambacho bidhaa yako inaenda kunifanyia.

 

 

Ukizungumzia kitu hicho ninachokihitaji halafu mwishoni ukaonesha kitu hicho nitakipata kupitia bidhaa yako basi sina budi kukutafuta uniuzie bidhaa yako.

 

 

Lakini ukizungumzia bidhaa yako hata sikuelewi maana unazungumza lugha isiyo eleweka kwenye ubongo wangu.

 

 

Usijisahaulishe kwamba hujui ubongo wangu saa zote unawaza kuhusu vitu ninavyovihitaji na sio vitu ambavyo watu wengine wanahitaji.

 

 

Kwanini nijali kuhusu bidhaa yako bila kuona umuhimu wa hiyo bidhaa kwangu?

 

 

Moving on…

 

 

Jambo #2: Maisha ya mteja yatakuwaje baada ya kununua bidhaa au huduma yako.

 

 

Kabla mteja hajanunua bidhaa yako kuna kitu anakikosa, si ndio?

 

 

Basi muelezee maisha yake yatakuwa na mabadiliko gani baada ya kupata bidhaa yako.

 

 

Kama nikinunua bidhaa yako sipati ongezeko lolote kwenye maisha yangu, kwanini sasa ninunue bidhaa yako?

 

 

Ongezeko linaweza kuwa furaha, pesa, mwonekano mzuri n.k 

 

 

Nitanunua bidhaa yako endapo utanionesha kwamba baada ya kununua bidhaa yako nitaondokana na kitu fuluni na nitapata kitu fulani kizuri zaidi kwenye maisha yangu.

 

 

Tunaelewana mpaka hapo?

 

 

Vizuri. Tumalizie…

 

 

Jambo #3: Mteja atapataje hitaji lake kupitia bidhaa yako?

 

 

Baada ya kuelezea kwamba kupitia bidhaa au huduma yako mteja atapata hitaji lake na ukaelezea ni utofauti gani bidhaa yako itauleta kwenye maisha yake…

 

 

Sasa ni wakati wa kumpa mteja wito wa kukupigia simu apate bidhaa yako, au aje whatsapp apate bidhaa yako….

 

 

Haijalishi ni sehemu ipi. 

 

 

Point ni kwamba unampa mteja maelekezo ya jinsi gani ataipata bidhaa yako.

 

 

Boom.

 

 

Mpaka hapo una tangazo makini sana la kukuletea utitiri wa watu ambao wapo tayari kununua bidhaa au huduma yako.

 

 

Usijifanye kipofu kwamba huoni ambacho mimi nimemaliza kukifanya kwako?

 

 

Nina darasa ambalo linafundisha kuhusu matangazo ya kulipia Facebook na Instagram.https://biashara-news.blogspot.com?m=1

 

 

Nina imani ningeanza post hii kwa kuzungumzia kuhusu darasa hili usingesoma mpaka mwisho.

 

 

Lakini kwakua najua hitaji lako ni wateja wengi mtandaoni nimeanza kwa kukufundisha kitu ambacho kitakusaidia kupata wateja hao ambacho ni uandishi wa tangazo lenye ushawishi.

 

 

Baada ya hapo nakupatia wito sasa ambao ni…

 

 

Kama unataka kujifunza kiundani njoo darasani sasa

https://biashara-news.blogspot.com/2023/05/andika-hivi-matangazo-yako-ya-mtandaoni.html



MAISHA NI MAFUPI

 Kuna mtu aliwahi kusema hivi

      "Life is short, live it. Love is rare, grab it. Anger is bad, dump it. Fear is awful, face it. Memories are sweet, cherish it."

  Akiwa na maana ya kusema kwamba;
"Maisha ni mafupi, yaishi. Upendo ni adimu kuupata, uchukue kwa haraka na ukamate. Maana yake ukipata anayekupenda usiruhusu akaenda zake Bali uhakikishe unamshikilia vilivyo.
       Hasira ni mbaya, itupe jalalani ili moyo wako uwe na Amani pamoja na Furaha kwa ajili ya kufurahia maisha aliyokupa Mungu.

        Hofu ni mbaya, ikabili alafu uishinde.

       Kumbukumbu ni tamu, zikumbuke sio uzikumbuke tu bali jifunze kutokana na kumbukumbu hizo ili nyakati zijazo uweze uweze kuwa bora zaidi ya zamani.

Kwahiyo hivyo vitu ukivifanyia kazi na kuvitekeleza hakika kuna mahali utaenda.

Philanthropist.



Ad